.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 21 Oktoba 2015

CANADA IMETHIBITISHA KUWA ITAZIONDOA NDEGE ZAKE ZA KIVITA SYRIA NA IRAKI

Waziri Mkuu mteuli wa Canada Justin Trudeau amethibitisha kuwa ataziondoa ndege za nchi yake zinazofanya mashambulizi ya anga dhidi ya kundi la Dola ya Kiislam (IS) nchini Irak na Syria.

Bw. Trudeau amemfahamisha rais Barack Obama juu ya uamuzi huo saa chache baada ya kukiongoza chama chake cha Liberal kushinda uchaguzi wa wabunge.

Ikiwa ni sehemu ya kampeni zake Bw. Trudeau aliahidi kuzirejesha nyumbani ndege zao za kivita za CF-18, ambazo zilipelekwa katika ukanda huo kushambulia IS hadi Machi 2016. Hata hivyo hajaeleza ataanza kufanya hivyo lini.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni