.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 21 Oktoba 2015

MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI BW. JOE BIDEN AMESEMA ALIUNGA MKONO OPERESHENI ILIYOMUUA OSAMA

Makamu wa rais wa Marekani Bw. Joe Biden amesema anaunga mkono operesheni ambayo ilifanikisha kuuwawa kwa kiongozi wa al-Qaeda Osama Bin Laden, akionesha kubadili msimamo wake wa awali.

Bw. Biden anafikiria kugombea urais wa Marekani na kauli yake ya awali inamfanya kuchukuliwa kama mtu ambaye anayesita kushambulia, ambapo pia anachukuliwa kama mwanasiasa mzigo.

Bw. Biden alinukuliwa akipendekeza rais Obama asifanye shambulizi hilo wakati akiongea na baraza la Congress mwaka 2012, kwa mujibu wa shirika la habari la ABC. Hata hivyo jana Bw. Biden amesema alimwambia rais kwa siri aendelee na mpango wa kumshambulia Osama.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni