.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 21 Oktoba 2015

VIONGOZI SITA WA KANISA MOJA KUBWA LA NCHINI SINGAPORE HATIANI KWA KUIBA FEDHA

Viongozi sita wa kanisa moja kubwa la nchini Singapore wametiwa hatiani kwa kosa la kujipatiwa kwa njia za udanganyifu fedha za kanisa zinazofikia kiasi cha dola milioni 50.

Hukumu ya Jaji imesema mchungaji wa kanisa hilo la City Harvest, Bw. Kong Hee pamoja na wenzake walitumia fedha za kanisa kumsaidia kimuziki mkewe Sun Ho ambaye ni mwimbaji wa muziki wa kidunia.

Katika utetezi wao viongozi wa kanisa hilo wamesema kuwa walitumia fedha hizo kumsaidia kukua kimuziki Bi. Ho ambaye ni mwanamuziki wa pop ili kuweza kutumia muziki wake kuwafikia watu wasio waumini wa dini ya kikristo.

Viongozi hao sita wa kanisa waponje kwa dhamana hadi hapo watakaposomewa adhabu yao, hata hivyo wanakabiliwa na adhabu ya kifungo jela kinachoweza kuwa cha maisha.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni