.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 20 Oktoba 2015

FAMILIA YA MWANARIADHA OSCAR PISTORIUS YAFURAHIA KURUDI NYUMBANI

Familia ya Oscar Pistorius imeongea kwa mara ya kwanza furaha waliyonayo baada ya mwanariadha huyo kutoka gerezani baada ya kukaa mwaka mmoja kwa kosa la kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp.

Mwanariadha huyo ambaye ni mlemavu wa miguu yote miwili ametoka gerezani siku moja mapema na ataendelea katumikia adhabu ya kifungo cha miaka mitano akiwa nyumbani kwao Jijini Pretoria.

Inaaminika akiwa nyumbani ataweza kuogelea bwawani, kumpumzika katika bustani, kuangalia TV pamoja na kuweza kufanya mazoezi.
                      Nyumba atakayokuwa akikaa Pistorius akimalizia kifungo chake
                                                             Reeva Steenkamp akiwa na Oscar Pistorius 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni