.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 20 Oktoba 2015

CHAMA CHA LIBERALS CHA CANADA KIMEPATA USHINDI MKUBWA KATIKA UCHAGUZI WA WABUNGE

Chama cha Liberals cha Canada kimepata ushindi mkubwa katika uchaguzi wa wabunge, na kumaliza miaka tisa ya utawala wa chama cha Conservative, kwa mujibu wa matokeo ya awali.

Chama cha Liberals kinachoongozwa na Justin Trudeau kinaongoza kwa kupata ushindi kwenye wilaya 185 za uchaguzi.

Mtoto huyo wa aliyekuwa waziri mkuu wa Canada marehemu Pierre Trudeau sasa anatarajiwa kuunda serikali ya Canada, kwa mujibu ubashiri wa mtandao wa vyombo vya habari vya CBC na CTV.

Waziri Mkuu aliyemadarakani kwa sasa wa chama cha Conservative, Stephen Harper, ambaye chama chake kinaongoza kwenye wilaya 103 za kupigia kura, amekubali kushindwa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni