Kocha Jose Mourinho ameepuka
kutimuliwa kibarua baada ya kukutana na bodi ya timu ya Chelsea,
kufuatia kufanya vibaya kwa timu hiyo na kukubali kipigo cha mabao
3-1 kutoka kwa Southampton hapo jana.
Ilikuwa inahofiwa kuwa Mourinho
atafukuzwa kazi ya kuinoa Chelsea baada ya kukubali kipigo cha sita
katika msimu huu, ambapo yeye mwenyewe alionekana akimshawishi
mmiliki wa Chelsea, Roman Abramovich kumfukuza kazi baada ya mchezo
huo.
Badala yake bodi ya Chelsea imemtaka
kocha Mourinho aendelee kukaa madarakani na kubadili hali ya matokeo
mabaya ya timu hiyo, huku akiungwa mkono na bodi katika kufanya
mabadiliko.
Mourinho akiwashangaa wachezaji wa Chelsea wanavyovurunda uwanjani
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni