Mshambuliaji nyota wa Manchester
City striker Sergio Aguero amedhihirisha kuwa yeye ni miongoni mwa
wachezaji bora waliopo katika Ligi Kuu ya Uingereza kwa wakati huu
baada ya jana kucheka na nyavu mara tano.
Mchezaji huyo raia wa Argentina jana
alifunga mabao hayo matano dhidi ya Newcastle United na kuisaidia
timu yake kuibuka na uishindi wa mabao 6-1, katika mchezo wao wa Ligi
Kuu ya Uingereza.
Kwa kufunga magoli matano katika
mchezo mmoja Aguero amefikia rekodi iliyowekwa na wachezaji Andy
Cole, Alan Shearer, Jermain Defoe pamoja Dimitar Berbatov ambao nao
walifunga idadi hiyo ya magoli katika Ligi Kuu ya Uingereza.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni