.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 13 Oktoba 2015

MSTAAFU MUINGEREZA KUCHAPWA VIBOKO 360 KWA KUKUTWA NA WINE SAUDI

Mzee mstaafu raia wa Uingereza aliyekamatwa nchini Saudi Arabia akiwa na mvinyo wakutengeneza nyumbani anakabiliwa na adhabu ya kuchapwa viboko 360, jambo ambalo familia yake imesema litamsababishia kifo.

Mzee huyo Karl Andree, mwenye umri wa miaka 74, ameshatumikia adhabu ya zaidi ya mwaka mmoja jela tangu alipokamatwa na polisi wa Saudi Arabia wanaofuata taratibu za dini ya Kiislam.

Binti wa mzeee Andree, Kirsten Piroth ameliambia shirika la habari la BBC, kuwa baba yake ambaye anasumbuliwa na tatizo la aina tatu za saratani hatoweza kumudu adhabu hiyo ya kuchapwa viboko 360.

Ofisi ya Uingereza ya Mambo ya Nje imesema kuwa inajaribu kushughulikia suala la mzee huyo ili aachiwe huru mara moja.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni