Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) nchini, Awa Dabo (kulia) na Mkuu wa ofisi ndogo ya Umoja wa Mataifa Zanzibar, Anna Senga (katikati) wakimkaribisha mmoja wa wageni waalikwa katika sherehe za kutimiza miaka 70 tangu kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa iliyofanyika katika Hoteli ya Serena Shangani Mjini Zanzibar mwishoni mwa wiki.(Picha na Zainul Mzige wa Mo Dewjiblog
Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa visiwani Zanzibar wakibadilishana mawazo wakati wa kuwasili kwa wageni waalikwa kwenye sherehe hizo.
Kila mtu alikuwa na tabasamu la furaha....Happy Birthday #UN70
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (kulia) akiteta jambo na Mkuu wa ofisi ndogo ya Umoja wa Mataifa Zanzibar, Anna Senga.
Ofisa anayeshughulikia masuala ya ushirikiano wa WHO Zanzibar, Dkt. Ghirmay Andemichael (kushoto) akibadilishana kadi na mmoja wa wageni waalikwa (ambaye jina lake halikuweza kupatikana kirahisi).
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) nchini, Awa Dabo (kushoto) akifurahi jambo na Mgeni rasmi Waziri wa nchi Ofisi ya Rais, Kazi na Utumishi wa Umma, Haroun Ali Suleiman.
Mgeni rasmi Waziri wa nchi Ofisi ya Rais, Kazi na Utumishi wa Umma, Haroun Ali Suleiman (kulia) na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez wakizindua rasmi malengo ya Maendeleo Endelevu 17 ( SDGs) katika sherehe za kutimiza miaka 70 tangu kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa iliyofanyika katika Hoteli ya Serena Shangani Mjini Zanzibar mwishoni mwa wiki.
Fataki zikipamba uzinduzi huo, sasa yamezinduliwa rasmi.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Bw. Alvaro Rodriguez akitoa salamu za Umoja wa Mataifa katika sherehe za kutimiza miaka 70 tangu kuanzishwa kwa Umoja huo.
Baadhi ya wakuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa Dar na Zanzibar wakimsikiliza Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Bw.Alvaro Rodriguez (hayupo pichani) wakati akitoa salamu za UN katika sherehe za kutimiza miaka 70 tangu kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa iliyofanyika katika Hoteli ya Serena Shangani Mjini Zanzibar.
Mgeni rasmi Waziri wa nchi Ofisi ya Rais, Kazi na Utumishi wa Umma, Haroun Ali Suleiman akitoa salamu za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika sherehe za kutimiza miaka 70 tangu kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa iliyofanyika katika Hoteli ya Serena Shangani Mjini Zanzibar.
Mgeni rasmi Waziri wa nchi Ofisi ya Rais, Kazi na Utumishi wa Umma, Haroun Ali Suleiman na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Bw.Alvaro Rodriguez pamoja na wakuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini wakifanya 'Toast' katika kilele cha sherehe za kutimiza miaka 70 tangu kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa iliyofanyika katika Hoteli ya Serena Shangani Mjini Zanzibar.
'Toast' hiyo iliambatana na milipuko ya Fataki kusherehesha miaka 70 ya Umoja wa Mataifa tangu kuanzishwa kwake. Kwa picha zaidi bofya link hii
Na Mwandishi wetu, Zanzibar
SERIKALI
ya mapinduzi Zanzibar imesema kuwa itaendelea kuthamini fursa mbali
mbali zinazotolewa na Umoja wa Mataifa (UN) ili ziweze kuwanufaisha
wananchi wote bila ya ubaguzi.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa
nchi Ofisi ya Rais, Kazi na Utumishi wa Umma, Haroun Ali Suleiman wakati
akihutubia katika sherehe za kutimiza miaka 70 tangu kuanzishwa kwa
Umoja wa Mataifa iliyofanyika katika Hoteli ya Serena Shangani Mjini
Zanzibar, alisema umoja huo umekuwa sekta muhimu ya kuunga mkono juhudi
za maendeleo ya serikali katika sekta mbali mbali za kiuchumi, kijamii
na kisiasa.
Alisema kuwa Zanzibar ikiwa miongozi mwa nchi
zinazoendelea barani Afrika inaendelea kutumia vizuri fursa zinazotolewa
na umoja huo kwa lengo la kujenga jamii bora zenye kipato na uwezo wa
kati kwa lengo la kupunguza umasikini nchini.
Waziri Haroun
alifahamisha kuwa miradi mbali mbali ya maendeleo inayotolewa na umoja
huo imekuwa nyenzo muhimu ya kuisaidia serikali kuhudumia wananchi wake
kwa ufanisi zaidi.
Alisema kutokana na misaada hiyo Zanzibar pia
imekuwa mdau muhimu wa umoja huo kwani ni miongoni mwa nchi yenye urithi
wa kimataifa kupitia maeneo ya Mji Mkongwe jambo ambalo ni ishara tosha
ya mahusiano mema kati ya umoja huo na serikali.
“
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inajali kwa kiasi kikubwa juhudi za
Umoja wa Mataifa kwa kutuunga mkono, nasi tunaendelea kutumia vizuri
miradi mnayotuunga mkono.
Pia tunaendelea kukuombeni mtusaidie
pale tutakapohitaji msaada wenu kwa Nyanja tofauti kwani bajeti ya
serikali haitoshi kukidhi mahitaji yote ya kuendesha serikali.”, Alisema
Waziri Haroun.
Naye Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa
Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro
Rodriguez alikiri kuridhishwa kwake na utekelezaji wa miradi mbali mbali
ya umoja huo na kuahidi kuendelea kushirikiana vizuri na serikali ili
kufikia dhana ya maendeleo endelevu Tanzania na Zanzibar kwa ujumla.
Bw.
Rodriguez alibainisha kuwa umoja huo bado unaendelea kufanya tathimini
na utafti juu ya masuala mbali ya kisiasa na kijamii nchini ili kuona ni
kwa jinsi gani watasaidia kuunga mkono maeneo hayo kwa maendeleo ya
nchi.
Alifafanua kuwa katika miradi mbali mbali iliyotekelezwa
Zanzibar kupitia mashirika ya Umoja huo hasa UNDP, UN WOMEN na UNESCO
miradi hiyo imeweza kufanikiwa zaidi ya asilimia 80 jambo ambalo ni
faraja kwa umoja huo.
Alieleza
kuwa kupitia dhana ya maendeleo endelevu kwa mwaka 2016 umoja huo
umejipanga kusaidia masuala mbali mbali ya haki za binadamu, utawala
bora, uwazi na uwajibikaji, afya na vipaumbele vya kisera kwa serikali
ili kuhakikisha Zanzibar inakuwa ni nchi ya kupigiwa mfano kimaendeleo.
“
Tuna kila sababu za kuishukru serikali ushiriki wake katika miradi yetu
kwani bila wao kutuunga mkono vizuri leo hii tusingweza kuwepo hapa
kusherekea mafanikio tuliyopata ndani ya miaka 70 ya UN hivyo nasi
tunaahidi kuenzi mahusiano haya kwa lengo la kujenga jamii bora.”,
alisema Bw.Rodriguez.
Aidha aliishauri serikali kuhakikisha
mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu unafanyika kwa amani na kwa
kuzingatia vigezo vya uwazi, uhuru na haki ili kila chama kilichoshiriki
katika mchakato huo kinapata haki yake kwa mujibu wa sheria za nchi.
“
Tunawatakieni uchaguzi mwema na wenye mafanikio bila ya kuwepo dalili
za uvunjaji wa haki za binadamu ama kiashiria chochote cha vurugu ili
muendelee kulinda heshima na mafanikio yaliyopatikana katika Serikali ya
Umoja wa Kitaifa (SUK).” alisisitiza Bw. Rodriguez.
Sherehe hizo
za kutimiza miaka 70 za UN zilifanyika katika ukumbi wa hoteli ya
Serena Mjini Zanzibar na kuwashirikisha wadau mbali mbali wa umoja huo
wakiwemo wawakilishi wa mashirika ya kimataifa yanayofanya kazi Zanzibar
na kutoa Tuzo na vyeti vya kumbu kumbu kwa taasisi na shule
zilizoshiriki kikamilifu katika utekelezaji wa baadhi ya miradi ya umoja
huo.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni