.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 14 Oktoba 2015

UCHUMI YATANGAZA KUFUNGA SUPAMAKETI ZAO TANZANIA NA UGANDA

Supamaketi ya Uchumi imetangaza kujiondoa kufanya biashara katika nchi za Tanzania na Uganda katika kusitisha upotevu zaidi wa fedha.

Mtendaji Mkuu wa Uchumi Supamaketi Bw. Julius Kipng'etich, amesema bodi ya kampuni hiyo imeamua kufunga maduka yake yote yakikanda ili kuimarisha shughuli zake za nchini Kenya.

Bw. Kipng’etich amesema Supamaketi zao za Tanzania na Uganda ni asilimia 4.7 tu ya maduka yake yote lakini zinagharimu asilimia 25 za gharama za uendeshaji.

Amesema maduka ya Uchumi ya mataifa hayo mawili ya Afrika Mashariki hayajaingiza faida kwa miaka mitano iliyopita, jambo ambalo linaonyesha yalikuwa yakinyonya fedha za makao makuu.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni