.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 7 Oktoba 2015

UMOJA WA ULAYA KUDHIBITI BOTI ZINAZOVYUSHA WAHAMIAJI

Umoja wa Ulaya unaanza operesheni mpya za kudhibiti boti zinazovusha wahamiaji kimagendo kukatiza bahari ya Mediterranean.

Chini ya Operesheni hiyo iitwayo Sophia, boti za vikosi vya wanamaji zitaruhusiwa kuingia, kufanya upekuzi, kuzikamata na kuzitimua boti zinazohisiwa kubeba wahamiaji.

Hadi sasa Umoja wa Ulaya umejikita katika uangalizi na operesheni za uokoaji wahamiaji ambao boti zao huzama mara kwa mara kutokana na kuwa duni na zenye kujaza mno watu.

Takwimu zinaonyesha zaidi ya wahamiaji na wakimbizi 130,000 wamekatiza Ulaya wakitokea pwani ya kaskazini mwa Afrika, huku wengine zaidi ya 2,700 wakifa maji.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni