.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 8 Novemba 2015

CHELSEA YAPATA KIPIGO CHA TATU MFULULIZO MOURINHO AKIWA HOTELINI

Golikipa wa timu ya Chelsea, Asmir Begovic, amesema kocha Jose Mourinho anaungwa mkono na wachezaji wake kuwa ni mtu sahihi anayeweza kubadili hali ya vipigo inayoendelea kuikabili timu hiyo.

Chelsea imepoteza mechi ya jana kwa kukubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Stoke City, ikiwa ni kipigo cha tatu mfululizo na kujikuta katika nafasi ya 16 katika msimamo wa Ligi Kuu ya Uingereza.

Katika mchezo huo Mourinho alikosa kuwepo uwanjani kufuatia adhabu ya chama cha Soka Uingereza kumfungia kutohudhuria mechi moja, badala yake alishuhudia mchezo huo akiwa hotelini.
Mashabiki wa Chelsea wakibebe picha ya Mourinho kudhihaki kuwa yupo uwanjani.

MAN U YAUONA MWEZI....
Kinda Jesse Lingard amefunga goli lake la kwanza katika Ligi Kuu ya Uingereza na kuisaidia Manchester United kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya West Brom katika mchezo uliochezwa kwenye dimba la Old Traffiord.

Jesse Lingard alipachika bao hilo zuri katika dakika ya 52, kwa shuti la kuzungusha, ambapo Juan Mata alipachika goli la pili kwa mkwaju wa penati baada ya Anthony Martial, kuchezewa rafu na Gareth McAuley aliyepewa kadi nyekundu kwa kosa hilo.
Matokeo mengine ya mechi za Ligi Kuu ya Uingereza ni, Bournemouth 0 - 1 Newcastle, Leicester 2 - 1 Watford, Norwich 1 - 0 Swansea, Sunderland 0 - 1 Southampton na West Ham 1 - 1 Everton.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni