.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 4 Novemba 2015

IKULU YA KENYA YASITA KUTHIBITISHA KENYATTA KUHUDHURIA KUAPISHWA DK. MAGUFULI

Ikulu ya Kenya imeendelea kuwa kimya iwapo rais Uhuru Kenyatta atahudhuria sherehe za kuapishwa rais mteule Dk. John Pombe Magufuli licha ya taarifa ya serikali ya Tanzania kusibitisha ujio wake.

Mkurugenzi Mwandamizi wa Mawasiliano ya Ikulu ya KenyaBw. Munyori Buku alipoulizwa na vyombo vya habari vya nchi hiyo jana kuhusu rais Kenyatta kuhudhuria sherehe hizo hakuthibitisha wala kukanusha suala hilo.

Taarifa ya serikali ya Tanzania imesema rais Kenyatta ataungana na viongozi Robert Mugabe wa Zimbabwe, Yoweri Museveni wa Uganda, Paul Kagame wa Rwanda, Jacob Zuma wa Afrika Kusini, Joseph Kabila wa (DRC), Filipe Nyusi wa Msumbiji pamoja na Edgar Lungu wa Zambia.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni