.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 17 Novemba 2015

MKUU WA MKOA KILIMANJARO, AMOS MAKALLA ATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA MLIMA KILIMANJARO


Duh, leo inanyesha kweli. Mkuu wa mkoa wa Kilimnajaro, Amos Makalla ( kushoto ) akiwa amejikinga na mvua alipowasili hifadhi ya Taifa ya mlima Kilimanjaro (KINAPA)

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Amos Makalla ametembelea Hifadhi ya Taifa ya mlima Kilimanjaro (KINAPA) na kufanya kikao na menejimenti ya  Kinapa, kukagua njia wanazopita watalii, utaratibu wa kuwapokea na kuwapandisha watalii mlima Kilimanjaro.
 Ameipongeza Kinapa kwa kuwa miongoni mwa hifadhi 5 zinazojiendesha vizuri na kuchangia mapato ya serikali, kuchangia ajira zaidi ya watu 100,000 kwa mwaka na usimamamizi madhubuti wa sheria za uhifadhi wa mazingira na kuanza kurejesha hali ya theluji ya mlima kilimanjaro iliyoanza kupungua kwa muda mrefu.

Katika ziara hiyo ameiagiza menejimenti kufanya yafuatayo:-
 
1. Kusimamia kwa nguvu zote eneo la hifadhi lisiingiliwe na shughuli za kilimo, ujangili man uharibifu wa vyanzo vya maji.
 
2. Kufanya mikutano na vijiji vyote 80 vinavyozunguka hifadhi kwa lengo la kuelimisha umma faida na hasara zitakazopatikana baada kuharibu mazingira.
 
3.Kuwafungia na kuwanyanganya leseni makampuni yanayopandisha watalii yanayotuhumiwa kwa udanganyifu , utapeli unaopelekea watalii kukosa huduma na kutapeliwa.
Aidha amewataka wananchi wa mkoa kilimanjaro kuendelea kupanda miti na kulinda mlima kilimanjaro na vyanzo vya maji

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni