.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 17 Novemba 2015

ULINZI MKALI KUELEKEA MECHI YA KIMATAIFA YA KIRAFIKI KATI YA ENGLAND DHIDI YA UFARANSA LEO USIKU

Ulinzi ukiwa umeimarishwa nje ya uwanja wa Wembley nchini Uingereza kabla ya mchezo wa kimataifa wa kirafiki utakaochezwa leo usiku katika uwanja huo baina ya wenyeji Uingereza dhidi ya Ufaransa.

Mchezo huo unachezwa zikiwa ni siku nne tu zimepita tangu mashambulio ya kigaidi yafanyike jijini Paris nchini Ufaransa ambapo jumla ya watu 129 waliuawa na wengine wengi kujeruhiwa.

Kikosi cha timu ya taifa cha Ufaransa kilisafiri kwenda London kuwavaa England katika mchezo huo wa kirafiki usiku wa leo baada ya kukataa kuahirisha kutokana na mashambulio ya kigaidi yaliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Paris.
Kikosi cha timu ya soka cha Ufaransa kikiwasili mapema leo asubuhi katika uwanja wa Wembley jijini London
         Ulinzi ukiwa umeimarishwa ndani ya uwanja wa Wembeley jijini London
Ulinzi ukiwa umeimarishwa nje ya uwanja wa Wembley jijini London nchini Uingereza.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni