.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 5 Novemba 2015

VIONGOZI MBALIMBALI WAENDELEA KUWASILI NCHINI KUSHUHUDIA UAPISHO WA RAIS MTEULE, MHE. DKT JOHN POMBE MAGUFULI


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (kushoto) akimpokea Rais wa Afrika ya Kusini Mhe. Jacob Zuma (anayeshuka kwenye ngazi), Rais Zuma amewasili nchini kwaajili ya kuudhuria sherehe za uapisho wa Rais Mteule Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli zitakazofanyika hapo kesho katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.

                                                               Waziri Membe akisalimiana na Rais Zuma


Rais Zuma akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini Mhe. Radhia Msuya (wa kwanza kulia).


             Rais Zuma akitizama kikundi cha ngoma kilichokuwa kikitoa burudani.


Balozi wa Tanzania nchini UAE Mhe. Mbarouk Nassoro Mbarouk (kushoto) akisalimiana na Waziri wa Maendeleo ya Jamii UAE.

Afisa Mambo ya Nje Bw. Hangi Mgaka naye akisalimiana na Waziri wa Maendeleo ya Jamii UAE.

                                                                                               Picha na Reginald Philip.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni