.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 2 Novemba 2015

WATU WANNE WAUWAWA KINYAMA MKAONI KAGERA

Watu wasiofahamika wanatafutwa na jeshi la polisi mkoani Kagera, kutokana na kusababisha vifo vya watu wanne waliokatwakatwa mapanga na miili yao kufunikwa na majani ya migomba.

Mauaji hayo yalitokea usiku wa kuamkia leo katika kijiji Ilogelo kata Katoma wilaya ya Bukoba, baada ya watu wasiojulikana awali kuwavamia watu wawili na kuwaua kwa kuwafyeka kwa mapanga kabla ya kufanya mauaji kama hayo kwa watu wengine wawili katika kata hiyo.

Kamanda wa polisi mkoani Kagera, Augustini Ollomi, aliwataja waliouawa katika matukio hayo ni Kaijage John (30), Anastella Paschal (42), Emmanuel Joseph (30) na Evodius Alloyce ambaye umri wake haujatambulika wote wakiwa wa kijiji cha Illogelo.

Kamanda Ollomi alisema, awali wauaji hao walianza kutekeleza mauaji yao kwa watu wawili (Kaijage John na Anastella Paschal), ambao walikumbwa na umauti huo wakati wakitoka matembezini na kurejea nyumbani.

Watu wasiofahamika wanatafutwa na jeshi la polisi mkoani Kagera, kutokana na kusababisha vifo vya watu wanne waliokatwakatwa mapanga na miili yao kufunikwa na majani ya migomba.

Mauaji hayo yalitokea usiku wa kuamkia leo katika kijiji Ilogelo kata Katoma wilaya ya Bukoba, baada ya watu wasiojulikana awali kuwavamia watu wawili na kuwaua kwa kuwafyeka kwa mapanga kabla ya kufanya mauaji kama hayo kwa watu wengine wawili katika kata hiyo.

Kamanda wa polisi mkoani Kagera, Augustini Ollomi, aliwataja waliouawa katika matukio hayo ni Kaijage John (30), Anastella Paschal (42), Emmanuel Joseph (30) na Evodius Alloyce ambaye umri wake haujatambulika wote wakiwa wa kijiji cha Illogelo.

Ollomi alisema, awali wauaji hao walianza kutekeleza mauaji yao kwa watu wawili (Kaijage John na Anastella Paschal), ambao walikumbwa na umauti huo wakati wakitoka matembezini na kurejea nyumbani.

Alisema mara baada ya wauaji hao kutekeleza unyama huo, waliifunika miili ya marehemu hao kwa kutumia majani ya migomba kisha kwenda kufanya mauaji kama hayo kwa (Joseph na Alloyce) na kuwafunika kutumia majani hayo ya mgomba.

Kutokana na mauaji hayo ya kinyama, jeshi la polisi linaendesha msako wa kuwatafuta wauaji hao huku likiomba msaada kutoka kwa raia wema, viongozi wa dini na wa serikali ili kutoa taarifa sahihi zisizo na nia ya kuoneana juu ya wahusika waliotenda unyama huo kwa lengo la sheria kufuata mkondo wake.

Hata hivyo, Ollomi alisema wahusika wa mauaji hao si wageni katika mkoa huo, hivyo kuwaomba wananchi kushirikiana vizuri na polisi na muda si mrefu wanaweza kupatikana ili hatua za kishera zichukue mkondo wake.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni