Eneo la kilomita 8 la Mto
Mississippi karibu na St Louis, Missouri, limefungwa kutotumiwa na
vyombo vya baharini kutokana na kuongezeka kwa maji katika kiwango
hatari.
Vikosi vya ulinzi vya majini
vimesema mvua ya gharika imeleta athari katika ukanda huo kwa siku
kadhaa, na kufanya mito kufurika maji.
Gavana wa Missouri, Jay Nixon,
amesema watu 13 katika jimbo hilo la Marekani wamekufa kutokana na
mafuriko.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni