Mshambuli wa Leicester City Jamie
Vardy na Riyad Mahrez wameisaidia timu yao kurejea kileleni mwa ligi
kuu ya Uingereza na kuisukuma chini zaidi ya msimamo wa ligi timu ya
Chelsea.
Katika mchezo huo ambao Chelsea
ilikuwa ugenini ilijikuta ikifungwa bao la kwanza na Jamie Vardy
katika dakika ya 34, kabla ya Riyad Mahrez kupachika la pili dakika
ya 48, huku Loic Lemy akiipatia Chelsea bao pekee la kufutia machozi.
Baada ya kipigo hicho cha mabao 2-1
kocha wa Chelsea Jose Mourinho amesema anajihisi kama kazi yake
inahujumiwa, huku akishuhudia akipoteza mchezo wa tisa kati ya
michezo 16 ya Ligi Kuu ya Uingereza.
Jamie Vaedy akipachika bao la kwanza kwa Leicester City
Benchi la ufundi la Chelsea likiwa hoi pamoja na wachezaji wa akiba



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni