Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani,
John Kerry, yupo Jijini Moscow kufanya mazungumzo ya kujaribu kuondoa
tofauti na Urusi kuhusiana na mchakato wa kisiasa wa kumaliza vita
nchini Syria.
Bw. Kerry anatarajia kukutana na
rais wa Urusi, Vladimir Putin, pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa
nchi hiyo Bw. Sergei Lavrov kuzungumzia suala hilo.
Marekani inataka rais Assad ajiuzulu
wakati Urusi ikisema uamuzi huo waachiwe wananchi wa Syria wenywe.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni