Mtoto wa Osama Bin Laden ameripotiwa
kuiomba Marekani cheti cha kifo cha baba yake, kwa mujibu wa tovuti
ya Wikileaks.
Barua hiyo kutoka Ubalozi wa
Marekani nchini Saudi Arabia ni miongoni mwa nyaraka 60,000 za
serikali ya Saudi Arabia zilizotolewa na Wikileaks.
Mwambata wa Kijeshi wa Ubalozi
Jenerali Glen Keiser alimuandikia Abdullah Bin Laden mwaka 2011
kumuambia kuwa hawezi kutoa cheti cha kifo cha Osama.
Tovuti hivyo ya kufichua siri za
mataifa mbalimbali ya Wikileaks imetoa nyaraka 500,000 inazodai ni za
serikali ya Saudi kwa mataifa ya kigeni.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni