.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 21 Desemba 2015

REAL MADRID YAFANYA MAUAJI MAKUBWA KATIKA MCHEZO WA LA LIGA

Gareth Bale ametikisa nyavu mara nne wakati Real Madrid ikifanya maafa makubwa ya funga mwaka kwa Rayo Vallecano kwa kuichakaza kwa magoli 10-2 katika Ligi ya La Liga.

Katika mchezo huo Real ili kuwa nyuma kabla ya mchezaji wa Vallecano Tito kutolewa kwa kadi nyekundu, licha ya Danilo kuifungia goli la kwanza kabla ya Antonio Amaya na Jozabed.

Bale alisawazisha kwa goli la kichwa kabla ya Raul Baena kutolewa nje kwa kadi nyekundu na Cristiano Ronaldo kufunga kwa mkwaju wa penati.

Baadae Bale akaongeza mabao matatu zaidi, Ronaldo akafunga lapili na Karim Benzema kufunga mabao matatu yaani hat-trick na idadi ya mabao kuwa 10-2.

Katika matokeo mengine Málaga 1 - 0 Atl Madrid, Ath Bilbao 2 - 0 Levante, Granada CF 0 - 2 Celta de Vigo na Real Sociedad 0 - 2 Villarreal.
                                            Gareth Bale akishangilia baada ya kucheka na nyavu 
            Cristiano Ronaldo akiwa juu angani kupiga mpira kwa kichwa na kufunga bao

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni