.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 21 Desemba 2015

STEVE HARVEY ACHANGANYA MAMBO SHINDANO LA MREMBO WA DUNIA

Mshereheshaji wa Shindano la Mrembo wa Dunia Steve Harvey ameomba radhi kwa kumtaja mrembo ambaye si mshindi Miss Ariadna Gutierrez kutoka Colombia kuwa ni mshindi.

Baada ya kosa hilo, Miss Ariadna Gutierrez alitangazwa kuwa ni mshindi wa pili na kulazimika kukabidhi taji alilovishwa kwa mrembo kutoka Philippines, Miss Pia Alonzo Wurtzbach.

#MissUniverse2015 imekuwa ni moja ya trendi usiku wa jana huku watumiaji wa mitandao ya jamii wasiamini kilichotokea.

Miss Wurtzbach aliwaambia waandishi anamtakia hali njema Miss Gutierrez.
                           Miss Ariadna Gutierrez akivuliwa taji alilokuwa amevishwa 
                                       Miss Philippines Pia Alonzo Wurtzbach akivishwa taji

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni