.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 14 Januari 2016

ARSENAL, CHELSEA NA MANCHESTER CITY ZABANWA MBAVU LIGI KUU YA UINGEREZA

Nafasi ya Arsenal ya kuongoza msimamo wa Ligi Kuu ya Uingereza kwa tofauti ya pointi, iliota mbawa jana baada ya Joe Allen kuisawazishia Liverpool na kuipatia pointi moja muhimu kwenye dimba la Anfield.

Katika mchezo huo ulioishia kwa sare ya mabao 3-3 Oliver Giroud alipachika wavuni mabao 2 na kukosa moja la wazi na kufanya idadi ya mabao aliyofunga katika msimu huu kufikia 18, wakati Arsenal ikiwa inaongoza kwa mabao 3-2 kabla ya Liverpool kusawazisha dakika ya 90.
    Kocha wa Arsenal Arsene Wenger akiduwaa baada ya koporwa ushindi dakika za mwisho.
                        Soka sio lelemama Diego Costa na McAULEY wakianguka chini

Katika mchezo mwingine bao la kusawazisha katika dakika za mwisho la James McClean, limeipora ushindi Chelesea na kuipatia pointi moja West Brom katika mchezo ulioishia kwa sare ya mabao 2-2 katika dimba la Stamford Bridge.
                                                 Refa akimzuia Diego Costa asipigane na Olsson

Matokeo mengine ya mechi za Ligi Kuu ya Uingereza jana Man City 0 - 0 Everton, Southampton 2 - 0 Watford, Stoke 3 - 1 Norwich, Swansea 2 - 4 Sunderland na Tottenham 0 - 1 Leicester.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni