.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 14 Januari 2016

GAVANA AMTUMIA KANSELA ANGEL MERKEL BASI LILILOJAA WAHAMIAJI OFISINI KWAKE

Mwanasiasa wa Bavaria aliyeonyesha kukerwa ametuma basi lililojaa wahamiaji 31 katika safari ya saa saba kwenda kwenye ofisi ya Angel Merkel Jijini Berlin baada kumuonya kiongozi huyo wa Ujerumani kuwa nchi imeelemewa na wahamiaji.

Wahamiaji hao walipakiwa kwenye basi aina ya Coach, huko Landshut mji wa kusini wa Bavaria na gavana Peter Dreir na kuwasafirisha maili 340 hadi katika mji mkuu wa Ujrumani, Berlin.


Dreier ambaye ni mkosoaji wa sera za Kansela Merkel za kuwapokea wahamiaji kwa kusema nchi hiyo imezidiwa na wahamiaji, amesema alishamtahadharisha Kansela huyo mwezi Oktoba mwaka jana.
Wahamiaji wakiwa wamepandishwa kwenye basi kwa safari ya kupelekwa ofisini kwa Kansela Angel Merkel

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni