Muwania urais wa Marekani kwa tiketi
ya chama cha Democratic Bi. Hillary Clinton amesema kumteuwa rais
Barack Obama kuwa jaji wa mahakama kuu ni wazo zuri kabisa.
Akiwa katika kampeni zake huko Iowa,
mpiga kura alimuuliza Bi. Clinton kama atafikiria kumteuwa rais Obama
kuwa jaji wa mahakama kuu iwapo atachaguliwa kuwa rais.
Bi. Clinton alikiri kuwa rais ajaye
atapatiwa fursa ya kuwachagua majaji watatu wa mahakama kuu, na
kumchagua rais Obama ni wazo zuri, ambalo hakuna mtu aliyewahi
kupendekeza kwake hapo kabla.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni