Michuano ya Olimpiki itakayofanyika
Rio nchini Brazili inakabiliwa na hofu ya ongezeko la virusi vya Zika
vilivyosababisha watoto 4,000 kuzaliwa na vichwa vidogo nchini humo.
Watanzamaji wanawake na wanariadha
waliokatika umri wa kupata ujauzito wametahadharishwa na wataalam wa
masuala ya afya duniani kufikiria vyema mipango yao ya kwenda Brazili
kutokana na hofu ya watoto watakaowazaa kukabiliwa na ugonjwa huo.
Urusi na Australia wameonyesha hofu
kwa wanamichezo wanawake wanaojiandaa kwa michuano ya Olimpiki
itakayofanyika Rio mwezi Agosti, huku mashirika kadhaa ya ndege
yakiwapa fursa wanawake wajawazito waliokata tiketi kuhudhuria
michuano hiyo kuziuza kwa watu wengine.
Mtu akinyunyuzia dawa ya kuulia mazalia ya mbu katika moja la eneo la viwanja vya michezo
Daktari akimpima ukubwa wa kichwa mtoto aliyezaliwa nchini Brazil



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni