Hoteli moja maarufu ya ufukweni
katika Jiji la Mogadishu nchini Somalia imekumbwa na mashambulio ya
milipuko iliyowekwa kwenye magari.
Bomo la kwanza la kwenye gari
lililipuka jana jioni na kufuatiwa na washambulia wenye silaha
waliokuwa wakitokea ufukweni, na kisha gari lingine kulipuka baadae
baada ya nusu saa.
Kunataarifa watu watatu wamekufa na
inahofiwa idadi ya vifo kuongezeka. Kundi la Al-Shabaab limesema
linahusika na shambulizi hilo na wapiganaji wake bado wapo kwenye
hoteli hiyo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni