Mchezaji aliyetokea benchi Charlie
Austin amefunga bao ndani ya dakika saba akiichezea kwa mara ya
kwanza Southampton na kupelekea wachezaji wa Manchester United watoke
dimbani wakizomewa na mashabiki wao baada ya kulala kwa bao moja kwa
bila.
Austin aliruka juu na kupiga mpira
wa kichwa uliozaa goli akiunganisha mpira wa adhabu uliopigwa katika
dakika ya 87, na kuifanya Southampton kuibuka na ushindi huo kwenye
dimba la Old Trafford, katika mchezo huo uliokuwa na nafasi chacheza
kufunga.
Charlie Austin akiruka na kufunga mpira wa kichwa uliomshinda David De Gea
Katika mchezo huo magoli ya Norwich
yalifungwa na Mbokani Bezua 29′, Naismith 41′ Hoolahan 54′,
(pen) Bassong 90′, huku ya Liverpool yakifungwa na Firmino 18′,
63′ Henderson 55′, Milner 75′ na Lallana 90′.
Dieumerci Mbokani akifurahia bao lake la kusawazisha alilolifunga kwa kisigino cha ufundi. Mchezo huo uliishia Liverpool 5-4 Norwich.
Matokeo Mengine ya Ligi Kuu ya
Uingereza ni Crystal Palace 1 – 3 Tottenham, Leicester 3 - 0
Stoke, Sunderland 1 - 1 Bournemouth, Watford 2 - 1 Newcastle, West
Brom 0 - 0 Aston Villa na West Ham 2 - 2 Man City.



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni