.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 24 Januari 2016

POLISI KENYA WANAMSAKA MUAJI ANAYEUWA MADADA POA TU

Mtu anayeendesha mauaji wa mfululizo katika Mji wa Nakuru nchini Kenya, yanayowalenga wanawake wanaojiuza miili yao bado hajapatikana kwa miezi mitatu, ambapo wanawake saba wanaojiuza wameshauwawa tangu Oktoba mwaka jana hadi Januari hii.

Maafisa polisi wanaochunguza mauaji hayo walimkamata mwanamke mmoja Januari 13 na kumshikilia kwa siku mbili na kumuachia, na jumatatu ya Januari 18 polisi walimkamata mwanaume mmoja kwa kuhusika na mauaji hayo ambaye bado anashikiliwa.

Hii si mara ya kwanza Kenya kutokea uhalifu wa muaji ya mfululizo yanayowalenga wanawake wanaojiuza miili yao. Mwaka 2010 mtuhumiwa Philip Onyancha alikiri mahakamani kuwa aliwauwa watu 19, wengi wao wakiwa ni makahaba na kisha kunywa damu zao.

Onyancha aliyefanya mauaji hayo kwa muda wa mwaka mmoja, alitiwa hatiani na mahakama na kuhukumiwa kifungo cha miaka 12 jela.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni