Mtu anayeendesha mauaji wa mfululizo
katika Mji wa Nakuru nchini Kenya, yanayowalenga wanawake wanaojiuza
miili yao bado hajapatikana kwa miezi mitatu, ambapo wanawake saba
wanaojiuza wameshauwawa tangu Oktoba mwaka jana hadi Januari hii.
Maafisa polisi wanaochunguza mauaji
hayo walimkamata mwanamke mmoja Januari 13 na kumshikilia kwa siku
mbili na kumuachia, na jumatatu ya Januari 18 polisi walimkamata
mwanaume mmoja kwa kuhusika na mauaji hayo ambaye bado anashikiliwa.
Hii si mara ya kwanza Kenya kutokea
uhalifu wa muaji ya mfululizo yanayowalenga wanawake wanaojiuza miili
yao. Mwaka 2010 mtuhumiwa Philip Onyancha alikiri mahakamani kuwa
aliwauwa watu 19, wengi wao wakiwa ni makahaba na kisha kunywa damu
zao.
Onyancha aliyefanya mauaji hayo kwa
muda wa mwaka mmoja, alitiwa hatiani na mahakama na kuhukumiwa
kifungo cha miaka 12 jela.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni