Mchekeshaji nyota Chris Rock
atasherehesha hafla ya utoaji tuzo za Oscars, licha ya kuwepo kwa
uvumi kwamba atajiondoa kutokana na waandaaji wake kudaiwa kuonyesha
upendeleo kwa waigizaji filamu weupe.
Prodyuza wa Tuzo za Oscars, Reginald
Hudlin, akiongea wakati wa uteuzi wa tuzo za 47 za NAACP jumamosi
Jijini Los Angeles amesema kuwa Rock, 50, atatekeleza majukumu yake
ya ushereheshaji tuzo hizo Februari 28.
Mchekeshaji huyo ambaye pia ni
muigizaji filamu atasherehesha tuzo hizo za Oscars, huku baadhi ya
wasanii wa tasnia ya filamu wenye asili ya Afrika kama, Muongoza
filamu Spike Lee, waigizaji Jada Pinkett Smith, na Will Smith
wakihamasisha kususiwa tuzo hizo.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni