.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 15 Januari 2016

MWANAMKE ALIYEOLEWA NA WANAUME WAWILI AFANIKIWA KUVUNJA NDOA MOJA

Matumaini ya mwanamke wa Mombasa Kenya aliyeolewa na wanaume wawili ya kutaka kutengana na mume wake wa kwanza ambaye mapenzi yamechuja, yamefanikiwa baada ya mahakama kuridhia kuvunja ndoa yake hiyo.

Hata hivyo, hukumu ya Mahakama ya Kadhi imemuagiza mwanamke huyo Rehema Dzuya kurejesha mahari ya samani za ndani zenye thamani ya shilingi 40,000 za Kenya alizotoa mumewe kama mahari.

Hata hivyo mume wa Rehema, Salim Twota amepinga maamuzi hayo ya Mahakama ya Kadhi, kwa madai kuwa yamempendelea mkewe, na kukesma atakata rufaa katika Mahakama Kuu kwa kuwa bado anampenda mkewe.

Kadhi Mkuu wa Mombasa Abdulhamin Athman amevunja ndoa hiyo kwa kusema ni vigumu sana kwa Rehema na mumewe Salim kuishi pamoja.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni