.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 14 Januari 2016

MWANAMKE AMUUA MPENZI WAKE KUTOKANA NA UGOMVI WA RIMOTI

Polisi Kenya inamshikilia mwanamke anayedaiwa kumuua mwanaume wake kwa kumchoma kisu, kufuatia ugomvi uliosababishwa na mvutano wa kuangalia programu za televisheni.

Kamishna wa Polisi wa Nairobi Kaunti Japhet Koome, amesema mwanamke huyo wa miaka 27 aitwae Caroline alimchoma mpenzi wake mwenye umri wa miaka 25 siku ya jumanne usiku.

Bw. Koome amesema wapenzi hao wawili walikuwa wanagombea remoti kila mtu akitaka kuangali programu tofauti na ndipo mwanamke alipochukua kisu jikoni na kumchoma nacho mwanaume tumboni na kwenye paja.

Ugomvi huo ulitokea saa nne usiku wakati chaneli moja televisheni ilipokuwa ikionyesha tamthilia na nyingine ikionyesha mechi ya mpira miguu.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni