Mwanamke Dorcas Awinja wa nchini
Kenya anauguliwa majeraha ya kuchomwa moto na mumewe kwa kutumia
mafuta ya taa, kutokana na ugomvi wa kusoma ujumbe wa simu wa nyumba
ndogo kwenye simu ya mumewe.
Awinja, amelazwa kwenye hospitali ya
Nairobi tawi la Nakuru mwili wake ukiwa umeungua kwa asilimia 63,
huku akiwa na majeraha ya kuungua na moto kwenye shingo, mkono, titi,
tumbo na miguuni.
Akisimulia kisa hicho Awinja amesema
wakati wakianza kulala simu ya mumewewe iliita bila ya kupokelewa na
ndipo alipoichukua ukaingia ujumbe wa mapenzi, uliomfanya apandwe
hasira na kuibua ugomvi, ulioishia yeye kuchomwa moto na mumewe.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni