.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 13 Januari 2016

NYUMBA YA GEORGE CLOONEY NA MKEWE AMAL YANYEMELEWA NA MAFURIKO

Nyumba ya nguli wa filamu George Clooney na mkewe mwanasheria wa haki za binadamu, Amal waliyoinunua kwa kiasi cha paundi milioni 10, inanyemelewa na mafuriko baada ya mto Themes kujaa maji na kupasuka kingo zake.

Nyumba hiyo ya nyota huyo wa filamu na mkewe iliyopo katika kijiji karibu na Reading, Berkshire nchini Uingereza ilikuwa imeshafanyiwa ukarabati wa vyumba vyake tisa, na sasa ipo hatarini iwapo mto Themes utafurika zaidi.


Kina chama maji cha mto Themes kimeongezeka mno baada ya wiki kadhaa za mvua na Mamlaka ya Mazingira Uingereza imeonya kutokea mafuriko katika maeneo yaliyo mabondeni hii leo.
        Maji ya mafuriko yakiwa yameshafika kwenye eneo la bustani la nyumba ya George Cloone
                                                                  George Clooney akiwa na na mkewe Amal

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni