Polisi nchini Afrika Kusini
wameanzisha uchunguzi wa vifo vya watoto watano ambao wanadhaniwa
walikufa kwa kukosa hewa baada ya kukutwa kwenye jokofu.
Watoto hao watano ndugu wenye umri
wa kati ya miaka mitatu na saba, waligunduliwa na Bibi yao kwenye mji
wa Kakamas, Kaskazini mwa Mkoa wa Cape siku ya Jumanne.
Katika tukio jingine watoto wawili
walikufa kwa kukosa hewa baada ya kufungiwa kwenye gari ambalo
lilikuwa linangojewa kufanyiwa matengenezo Jijini Johannesburg.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni