Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na wananchi wa Arusha
Mjini wakati akipita Barabarani kuelekea Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi
(TMA) Monduli ambako pamoja na mambo mengine kesho tarehe 23 Januari,
anatarajiwa kutunuku Kamisheni kwa Maafisa wanafunzi wa Chuo cha
Mafunzo ya Kijeshi Monduli kundi la 57/15.
Rais Dk. Magufuli akiwa amevalia
sare za kijeshi amesimamishwa na kuwasalimu wananchi katika maeneo ya
Sanawari, Tekniko, Ngarenaro, Mbauda, Majengo na Kisongo, Mkoani
Arusha.
Wakazi wa Arusha walijitokeza kwa wingi kumsikiliza Rais Dk. Magufuli, wakati walipomsimasha kuwasalimia kwa muda.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni