Rais wa Colombia Juan Manuel Santos
ametia saini sheria ambayo inatoa adhabu kali kwa wahusika wa matukio
ya mashambulizi ya kutumia tindikali.
Sasa mtu yeyote atakayetiwa hatiani
kwa kosa la kushambulia mtu kwa kutumia tindikali atahukumiwa kifungo
cha jela cha kati ya miaka 12 hadi 50.
Mashambulizi ya kutumia tindikali
yamekuwa yakitia hofu kubwa nchini Colombia kwa zaidi ya muongo
mmoja.
Watu wapatao 100 wengi wao wakiwa ni
wanawake wanakadiriwa kukumbana na mashambulizi ya kutumia tindikali
kila mwaka.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni