.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 19 Januari 2016

RAIS WA COLOMBIA ATIA SAINI SHERIA KALI YA KUWAADHIBU WANAOSHAMBULIA KWA TINDIKALI

Rais wa Colombia Juan Manuel Santos ametia saini sheria ambayo inatoa adhabu kali kwa wahusika wa matukio ya mashambulizi ya kutumia tindikali.

Sasa mtu yeyote atakayetiwa hatiani kwa kosa la kushambulia mtu kwa kutumia tindikali atahukumiwa kifungo cha jela cha kati ya miaka 12 hadi 50.

Mashambulizi ya kutumia tindikali yamekuwa yakitia hofu kubwa nchini Colombia kwa zaidi ya muongo mmoja.

Watu wapatao 100 wengi wao wakiwa ni wanawake wanakadiriwa kukumbana na mashambulizi ya kutumia tindikali kila mwaka.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni