.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 19 Januari 2016

SPIKE LEE NA JADA PINKETT SMITH KUSUSIA SHEREHE ZA TUZO ZA OSCARS

Nyota maarufu wawili wa masuala ya Wamarekani wenye asili ya Afrika wametangaza kususia kuhudhuria tuzo za Oscars kutokana na uteuzi wake kutowakilisha jamii zote.

Muongozaji filamu wa Spike Lee na muigizaji Jada Pinkett Smith wametuma ujumbe kila mmoja wakisema hawatahudhuria utoaji wa tuzo hizo zilizopangwa kufanyika Februari 28.

Tuzo za Oscar zimekumbana na kukosolewa baada ya kuteuliwa watu weupe pekee kuwania tuzo muhimu wakati zikitangazwa Alhamis, hali inayojionyesha kujirudia kwa mara ya pili tangu tuzo zilizopita.

Spike Lee ameandika kwamba hawezi kuunga mkono tena Oscars kwani wanachofanya ni kuwakosea heshima watu weusi na kuhoji kuwa inawezekanaji uteuzi wa wawania tuzo muhimu  20 za uigizaji wote ni watu weupe kwa mwaka wa pili mfululizo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni