Nyota maarufu wawili wa masuala ya
Wamarekani wenye asili ya Afrika wametangaza kususia kuhudhuria tuzo
za Oscars kutokana na uteuzi wake kutowakilisha jamii zote.
Muongozaji filamu wa Spike Lee na
muigizaji Jada Pinkett Smith wametuma ujumbe kila mmoja wakisema
hawatahudhuria utoaji wa tuzo hizo zilizopangwa kufanyika Februari
28.
Tuzo za Oscar zimekumbana na
kukosolewa baada ya kuteuliwa watu weupe pekee kuwania tuzo muhimu
wakati zikitangazwa Alhamis, hali inayojionyesha kujirudia kwa mara
ya pili tangu tuzo zilizopita.
Spike Lee ameandika kwamba hawezi
kuunga mkono tena Oscars kwani wanachofanya ni kuwakosea heshima watu
weusi na kuhoji kuwa inawezekanaji uteuzi wa wawania tuzo muhimu 20 za
uigizaji wote ni watu weupe kwa mwaka wa pili mfululizo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni