Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Misungwi mkoani Mwanza, Charles Kitwanga akipanda mti wa kumbukumbu katika eneo la Shule ya Msingi ya Ihelele iliyopo Kata ya Ilujamate, Wilaya ya Misungwi. Shule hiyo inajengwa kwa nguvu ya wananchi pamoja na kuchangiwa na Mamlaka wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira Kahama Shinyanga (KASHWASA) ambayo inamradi mkubwa wa maji katika Kijiji cha Ihelele ambapo shule hiyo inapojengwa.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Misungwi mkoani Mwanza, Charles Kitwanga akizungumza na wananchi wa Kata ya Misasi mara baada ya kukabidhi vitanda (20), magodoro (20) pamoja na shuka (20) katika Kituo cha Afya cha Misasi wilayani Misungwi. Waziri Chikawe katika hotuba yake aliwaahidi wananchi wa eneo hilo ujenzi wa barabara ya lami pamoja na upatikanaji wa maji.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Misungwi mkoani Mwanza, Charles Kitwanga akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhi misaada mbalimbali ikiwemo vitanda (20), magodoro (20) pamoja na shuka (20) katika Kituo cha Afya cha Misasi wilayani Misungwi. Picha zote na Felix Mwagara.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni