.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 13 Januari 2016

PAUL DUMMETT AINYIMA USHINDI MANCHESTER UNITED

Goli la dakika ya 90 la Paul Dummett liliifanya Newcastle kuinyima ushindi Manchester United ili kuweza kuwa na pointi sawa na Tottenham katika nafasi ya nne ya msimamo wa Ligi Kuu ya Uingereza.

Katika mchezo huo ulioishia kwa sare ya mabao 3-3, Wayne Rooney aliifungia Manchester united bao la kwanza kwa njia ya penati na kisha Jesse Lingard kuongeza la pili kabla ya Georginio Wijnaldum na Aleksandar kusawazisha.
         Wachezaji wa Manchester United wakishangilia bao lililofungwa na Wayne Rooney
                             Jesse Lingard akipachika bao la pili la Manchester United 
Katika mchezo mwingine timu iliyomkiani mwa msimamo wa ligi ya Aston Villa ilipata ushindi wake wa kwanza ikiwa chini ya Remi Garde baada ya kosa la kizembe lililofanywa na kipa wa Crystal Palace, Wayne Hennessey.

Hennessey aliruhusu kizembe mpira wa kona uliopigwa kichwa na Joleon Lescott kumpita na kuandika bao pekee katika mchezo huo wa Ligi Kuu ya Uingereza. Matokeo mengine ya jana ni Bournemouth 1 - 3 West Ham.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni