.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 13 Januari 2016

MAMIA YA NAKALA ZA BAJETI YA NIGERIA YA MWAKA 2016 ZAPOTEA BUNGENI

Mamia ya nakala za bajeti ya Nigeria ya mwaka 2016 zimepotea bungeni katika bunge la nchi hiyo, kwa mujibu wa mbunge mmoja ambaye hakutaka jina lake litajwe.

Baraza la Seneti la Nigeria limeshindwa kuanza kujadili pendekezo la bajeti hiyo kutokana na kupotea kwa nakala za bajei hiyo.

Kuchelewa kujadiliwa kwa bajeti hiyo kutachangia hali ya uchumi wa Nigeria kuwa mbaya zaidi, kutokana na taifa hilo kukumbwa na athari za kushuka kwa bei ya mafuta duniani.

Rais Muhammadu Buhari aliwasilisha nakala za bajeti yake hiyo ya kwanza tangu aingie madarakani kwa mabunge yote mwishoni mwa mwezi Desemba mwaka jana.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni