.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 8 Februari 2016

CHUI AINGIA KATIKA ENEO LA SHULE MJINI BANGALORE NA KUJERUHI WATU


Chui dume aliyeingia kwenye eneo la shule katika mji wa Bangalore nchini India amewajeruhi watu sita waliokuwa wakijaribu kumkamata.

Mwanasayansi mmoja na mtumishi wa misitu ni miongoni mwa watu waliong'atwa na chui huyo katika jitihada za kumkamata zilizodumu kwa saa 10 siku ya jana.

Chui huyo aliyeiingia kwenye shule ya Kimataifa ya Vibgyor, hatimae walifanikiwa kumlewesha kwa dawa za usingizi na kumkamata.

Sensa ya wanyamapori ya hivi karibuni nchini India inakadiria nchi hiyo ina chui kati ya 12,000 ama 14,000.
                 Mmoja wa majeruhi akipewa msaada wa kuondolewa sehemu ya tukio
   Baadhi ya watu wakikimbia kuokoa maisha yao baada ya chui kuanza kuwafuata

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni