.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 26 Februari 2016

KATIBU MKUU WA UN ATUA JUBA KUJARIBU KUTAFUTA MANI YA SUDANI KUSINI

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amewasili Juba katika kujaribu kufufua makubaliano ya amani ambayo yamekwama ili kumaliza miaka miwili ya mapigano ya wenyewe kwa wenyewe nchini Sudani Kusini.

Ki-moon alipokelewa jana uwanja wa ndege wa Juba na Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo Barnaba Marial Benjamin na kisha kupelekwa kuonana na rais Salva Kiir ambaye tafauti zao na mpinzani wake Riek Machar ziliibua machafuko tangu Desemba 2013.

Mapigano yanaendelea licha ya makubaliano ya amani ya Agosti mwaka jana ambapo watu wapatao 18 wameuwawa katika tukio la hivi karibuni kaskazini mashariki mwa mji wa Malakal wiki iliyopita.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni