Kinda mshambuliaji Marcus Rashford
amepachika mabao mawili akiichezea kwa mara ya kwanza timu ya wakubwa
ya Manchester United na kuing'oa nje ya michuano ya Ligi ya Uropa
hatua ya 16 bora.
Mabingwa hao wa Denmark walikuwa
wanaongoza kwa ushindi wa mabao 2-1 walioupata katika mchezo wao wa
awali, uliokuwa ukiwapa matumaini ambayo jana yaliyayuka baada ya
kuchapwa 5-1. Na kutolewa kwa tafuati ya magoli 6-3.
Katika mchezo huo mabao yalifungwa
na Bodurov aliyejifunga, Rashford dakika ya 63 na 75, Herrera kwa
penati dakika ya 87 na kisha Depay kukamilisha karamu ya magoli
katika dakika ya 90.
Memphis Depay akishangilia goli lake alilofunga dakika ya 90
Kocha Louis van Gaal akifuatilia mchezo huo pamoja na msaidizi wake Ryan Giggs



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni