Chama cha Soka cha Uingereza
kimesema ratiba ya michezo iliyofuatana kwa karibu haiwezi
kubadilishwa, hali inayokinzania na miongozo ya UEFA ili kuipa fursa
Arsenal na Hull kumaliza mchezo wa FA kwanza kabla ya usiku wa Ligi
ya Mabigwa Ulaya.
Mchezo wa marudio wa FA mzunguko wa
tano utakaoonyeshwa Live BT Sport, siku ya jumanne utagongana na
mechi ya Real Madrid na Roma pamoja na Wolfsburg na Gent za michuano
ya Mabingwa Ulaya.
Mchezo huo wa Arsenal na Hull
utakaopigwa kwenye dimba la KC stadium utaanza majira ya saa moja
usiku majira ya Uingereza, lakini hata hivyo kwa kufanya hivyo
inavunjwa sheria ya UEFA inayotaka michezo ya ndani kuisha dakika 30
kabla ya kuanza mchezo wa Mabingwa wa Ulaya.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni