.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 29 Februari 2016

KUNDI LA WAHAMIAJI LAVUNJA UZIO MPAKANI MWA MACEDONIA NA UGIRIKI

Kundi la wahamiaji limevunja kizuizi cha fensi ya waya zenye kuchoma kwenye mpaka wa Macedonia na Ugiriki wakitumia vyuma kuvunja uzio huo.

Picha za TV zimeonyesha wahamiaji wakisukuma uzio huo huko Idomen, na kuzikata nywaya za kuchoma huku polisi wa Macedonia wakitumia mabomu ya machozi kuwatimua.

Haijafahamika mara moja wahamiaji wangapi wameweza kuvuka, ambapo wengi wao wanataka kufika nchi za Ulaya wakitokea Syria na Irak.
    Wahamiaji wakisukumana na polisi wenye ngao za kioo baada ya kuvunja uzio huo
    Mtoto akiangua kilio wakati wa ghasia hizo zilizoambatana na mabomu ya machozi

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni