.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 29 Februari 2016

WAZIRI WAZAMANI WA MAMBO YA NDANI NIGERIA AFUNGULIWA MASHTAKA

Waziri wazamani wa mambo ya ndani wa Nigeria amefunguliwa mashtaka ya kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu kuhusiana na zoezi la ajira lililopelekea watu kukanyagana na kusababisha vifo vya watu 20.

Waziri huyo Abba Moro aliongoza zoezi hilo la kuwahamasisha wahitimu vijana wa vyuo vikuu kuomba nafasi za ajira kwenye idara ya uhamiaji mwaka 2014.

Uwanja uliotumika kwa usahili wa vijana wanaoomba ajira ulizidiwa na watu waliojitokeza kuomba ajira.


Bw. Moro amekiri kosa la kuhusika na kujipatia fedha kiasi cha dola milioni 2.5 kwa njia za udanganyifu zinazohusina na ada ya maombi ya kazi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni