Maelfu ya mashabiki wa timu ya
Liverpool walitoka nje ya uwanja wao jana wakati wa mchezo wao na
Sunderland katika dimba la Anfield kupinga kuongezwa kwa gharama za
tiketi.
Kundi hilo la mashabiki wa Liverpool
liliwahamasisha mashabiki kuondoka uwanjani dakika ya 77 ya mchezo
huo kupinga bei ya tiketi ya gharama ya juu kuuzwa paundi 77 kwenye
dimba lao jipya katika msimu ujao.
Katika mchezo huo ulioishia kwa sare
ya mabao 2-2 mashabiki wa Liverpool walitoka uwanjani wakiimba wimbo
wa klabu hiyo wa 'You'll Never Walk Alone', huku wakipaza sauti kwa
kusema bei hiyo mpya haiwezekani.
Shabiki wa Liverpool anayepinga bei mpya akiwa na ujumbe unaosema ni aibu paundi 77



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni