.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 10 Februari 2016

MAHAKAMA YAKWAMISHA MPANGO WA RAIS OBAMA KUDHIBITI HEWA UKAA

Mpango ya rais Barack Obama ya kudhibiti uchafuzi wa hewa ya ukaa kutoka kwenye mitambo ya nishati ya umeme ya Marekani umekwamishwa kwa muda na Mahakama ya Juu ya nchi hiyo.

Mahakama imesema mpango wa rais Obama wa matumizi ya nishati isiyochafua hewa, hauwezi kutekelezwa hadi hapo pingamizi la kisheria lililowasilishwa litakaposikilizwa.

Mpango huo wa rais Obama umeandaliwa kupunguza uchafuzi wa hewa Marekani kwa sailimia 32 ifikapo 2030, huku ukisisitiza matumizi ya nishati jadifu.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni